1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Martin Fayulu akataa mwito wa maridhiano wa Tshisekedi

3 Februari 2019

Kiongozi wa upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia Congo Martin Fayulu amekataa juhudi za rais mpya wa nchi hiyo Felix Tshisekedi za kutaka maridhiano.

DR Kongo Martin Fayulu in Kinshasa
Picha: Reuters/B. Ratner

Mwito huo wamaridhiano umetolewa na rais mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika jitihada ya kutafuta maridhiano ya kisiasa nchini humo.  Fayulu amesema pale unapopewa mkono ambao ni mchafu, hupaswi kuupokea.

Rais mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasiaya Kongo Felix TshisekediPicha: picture-alliance/dpa/B. Curtis

Kwenye hotuba yake rasmi ya kwanza tangu kushindwa kwenye uchaguzi wa rais, Fayulu aliwaambia mamia ya wafuasi wake waliokusanyika mjini Kinshasa, kuwa awasifanye fujo wakati anapoendelea kupinga uchaguzi anaodai ulikumbwa na udanganyifu. Kiongozihuyo wa upinzani ameuhimiza Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika kutopokea maagizo kutoka kwa mtu anayedai kuwa Wakongo hawakumchagua.

Mwandishi:John Juma/DPAE

Mhariri: Zainab Aziz

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW