1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Haki za binadamuJamhuri ya Kongo

DRC: Wakaazi wataka mamlaka kukabidhi maiti kwa familia zao

14 Septemba 2023

Familia za wahanga waliopoteza maisha katika maandamano ya dhidi ya vikosi vya MONUSCO, wameitaka mamlaka za mji wa Goma kuwakabidhi miili ya wapendwa wao kwa ajili ya mazishi.

Maandamano dhidi ya MONUSCO Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Maandamano dhidi ya MONUSCO Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoPicha: Moses Sawasawa/AP Photo/picture alliance

Vifo vya hivi karibuni vilivyotokea  mjini Goma tarehe 30 Agosti katika maandamano dhidi ya ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemocrasia ya Kongo MONUSCO, vimeacha familia nyingi zikiwa na huzuni kubwa, huku  wanavumilia maumivu yasiyoisha.

Baada ya wiki mbili,bado familia za wahanga wanangojea  kupewa miili ya watu wao kuwazika kwa heshima.

Kwa bahati mbaya, miili haikuwahi kupelekwa katika vyumba vya kuhifadhi maiti, jambo linaloongeza hatari ya kuoza kwa miili hiyo. 

Soma pia:Makamanda wawili wa jeshi wakamatwa Congo

Baadhi ya familia za wahanga waliopoteza maisha katika maandamano hayo, wameiambia DW kwamba, wanachohitaji kwa sasa ni miili hiyo kwa ajili ya shughuli za mazishi.

"Tunahitaji kuzika kwa heshima jamaa zetu." Alisema Laetitia Mazino katika mahopjiano na mwandishi wa Dw mjini humo.

Wakaazi hao wameitaka serikali kuingilia kati ili kumaliza kadhia hiyo ambayo wameitaja ni hatari pia kwa wakaazi wanaozunguka kambi hiyo, kutokana na miili hiyo kutohifadhiwa kwa kufuata miongozo ya afya.

Mashirika ya kiraia yaingilia kati

Miili ya wahanga wote iko nyuma ya kambi ya kijeshi ya Goma, imerundikwa ndani ya kontena. Hakuna aliyezikwa bado. 

Wakaazi Kivu washinikiza kuondolewa MONUSCO DRC

02:15

This browser does not support the video element.

Kwa mujibu wa mashirika la kiraia ya Goma, miili hiyo ambayo imeanza kuharibika inaleta hatarikubwa kwa afya ya watu wanaoishi karibu na kambi hii.

Marrion Ngavo, mkuu wa shirika la kiraia la Goma, anaiomba serikali iheshimu utu wa binadamu kwa kuzika miili hii. 

Soma pia:Watu wasiopungua kumi wauawa katika maandamano mjini Goma

Zaidi ya watu 130 wamekamatwa katika kesi hii na kufikishwa mbele ya mahakama katika kesi ya kisheria tangu wiki iliyopita. 

 Wito wa kutaka  hatua zichukuliwe  unazidi kuongezeka mjini Goma, na kuna matumaini kutoka kuchukua hatua kwa kutoa miili hiyoi kwa familia zao.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW