1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DRC yafurahia kukamatwa kwa Kabila

11 Februari 2013

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imeipongeza Afrika ya Kusini kwa kumkamata mtu anayejiita Etienne Kabila na watu wengine 19 waliokuwa wakipanga njama ya kuipindua serikali ya Rais Joseph Kabila.

Joseph Kabila
Joseph KabilaPicha: picture-alliance/dpa

Serikali ya Kongo imeomba watu hao kufikishwa kwenye vyombo vya kisheria nchini mwake ili kujibu makosa yao. Wakati huo huo, kiongozi mwingine wa kundi jipya la waasi la UFRC amekamatwa jimboni Kivu ya Kusini, wakati ambapo mjini Kinshasa juhudi za mjadala kwa ajili ya maridhiano ya kitaifa zimeanzishwa na chama tawala.

Sikiliza taarifa ya mwandishi wetu wa Kinshasa, Saleh Mwanamilongo, kwa kubonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW