Wanamgambo washambulia maeneo muhimu ya kijeshi Sudan
14 Septemba 2025
Matangazo
Afisa huyo amesema mashambulizi hayo yalilenga makao makuu ya jeshi la Sudan pamoja na maghala ya mafuta Magharibi mwa Mto Nile.
Mashambulizi mengine pia yalilenga kambi ya jeshi la anga la Kenana na uwanja mdogo wa ndege Kusini Mashariki mwa mji wa Kosti. Kituo cha umeme cha Um Dubakir pia kilishambuliwa.
Tangu Aprili mwaka 2023, Sudan imekuwa ikipambana na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya jeshi la taifa na wanamgambo wa kundi la RSF.
Vita hivyo hadi sasa vimesababisha mauaji ya maelfu ya watu huku mamilioni ya wengine wakipoteza makaazi yao.