1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DW Kiswahili yamuomboleza Mohammed Abdulrahman

16 Julai 2025

Idhaa ya Kiswahili ya DW inaomboleza kifo cha Mohamed Abdulrahman, mmoja wa nguzo muhimu wa Idhaa hii kwa zaidi ya miongo mitatu.

Timu ya DW Kiswahili ya miaka ya 80. Mohammed Abdulrahman wa mwanzo kushoto
Timu ya DW Kiswahili ya miaka ya 80. Mohammed Abdulrahman wa mwanzo kushotoPicha: DW

Mohammed aliaga dunia usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake mjini Cologne, Ujerumani. Kabla ya kustaafu mwaka 2019, Mohamed alikuwa Naibu Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili na mhariri maarufu aliyetoa mchango mkubwa kwa kizazi cha wanahabari.

Waliomfahamu wanamkumbuka kama mwandishi mahiri, mlezi, na mjenzi wa Kiswahili fasaha na sanifu ndani ya DW. Alijulikana si tu kwa sauti yake hewani, bali kwa umahiri wake wa kuandika na kufundisha. Mohammed Abdulrahman ameacha alama isiyofutika.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW