1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Elon Musk kushitakiwa Brazil

8 Aprili 2024

Jaji wa Mahakama ya Juu ya Brazil, Alexandre de Moraes, ameanzisha uchunguzi dhidi ya mmiliki wa mtandao wa kijamii wa X, Elon Musk.

Mmiliki wa mtandao wa kijamii wa X, Elon Musk.
Mmiliki wa mtandao wa kijamii wa X, Elon Musk.Picha: Gonzalo Fuentes/REUTERS

Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, Musk anatuhumiwa kwa kuzuwia sheria kuchukuwa mkondo wake.

Mmiliki huyo wa mtandao wa X anapingana na uamuzi wa Jaji Moraes ulioutaka mtandao huo wa kijamii kuzifungia baadhi ya akaunti za watumiaji.

Soma zaidi: Twitter yaondowa alama ya buluu kwenye akaunti za watu mashuhuri

Mapema hapo jana, Musk alituma ujumbe kwenye mtandao huo akisema X itaondowa zuio dhidi ya watumiaji hao kwa kuwa ni kinyume na katiba.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW