1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Macron aanza ziara ya siku tatu Uingereza

8 Julai 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameanza ziara ya siku tatu nchini Uingereza. Katika ziara hiyo Macron kupitia mwaliko wa Mfalme Charles III atalihutubia bunge na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu Keir Starmer.

Macron yuko ziarani Uingereza
Rais wa Ufaransa Emmanuel MacronPicha: dts-Agentur/picture alliance

Kando ya kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo, Starmer na Macron watazungumzia masuala mbalimbali ikiwemo kuongeza bajeti ya ulinzi na juhudi za pamoja za kukabiliana na wahamiaji haramu.

Macron atakutana pia Mwanamfalme William na mkewe kabla ya kuelekea katika Kasri la Windsor kukutana na Mfalme Charles na mkewe Camilla.

Starmer na Macron wanatarajiwa kufanya mkutano na nchi washirika Alhamisi 10.07.2025 kujadili msaada zaidi kwa Ukraine na namna ya kuishinikiza zaidi Urusi katika vita vyake dhidi ya Ukraine. Watazungumza na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na Waziri Mkuu wa Italia Giorgia Meloni.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW