1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUturuki

Erdogan aonya Sweden kuhusu NATO baada ya kuchomwa Quran

24 Januari 2023

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameionya Sweden kwamba hatounga mkono juhudi zake za kujiunga na Jumuiya ya NATO kufuatia tukio la kuchoma Qur'an nje ya ubalozi wa Ankara mjini Stockholm.

 Recep Tayyip Erdogan
Picha: Emin Sansar/AA/picture alliance

Kauli za hasira zilizotolewa na Rais Erdogan zimezidi kuyafifisha matarajio ya Sweden na Finland kujiunga na muungano huo wa ulinzi wa mataifa ya magharibi, kabla ya uchaguzi wa rais na bunge nchini Uturuki wa mwezi Mei.

Erdogan amesema ikiwa Sweden inawapenda sana wanachama wa mashirika ya kigaidi na maadui wa Uislamu, basi ipeleke masuala ya usalama wake kwao.

Marekani imesema tukio hilo la kuchukiza la kuchomwa Quran lililofanywa na mfuasi wa itikadi kali za mrengo wa kulia huenda lililenga kuhujumu umoja ndani ya NATO.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW