1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Erdogan kumshawishi Putin kufufua mkataba wa nafaka Ukraine

4 Septemba 2023

Rais wa Urusi Vkadmir Putin ameshikilia msimamo wake kwamba nchi yake hatorudi kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka kupitia bahari nyeusi mpaka masharti yote ya mkataba huo yatakapozingatiwa.

Russland Sotschi Türkei Erdogan Putin
Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan akiwa na mwenzake wa Urusi Vladimir PutinPicha: Sergei Guneev/Sputnik/REUTERS

Urusi inadai nchi za Magharibi zinapaswa kuiondolea vikwazo vinavyoharibu biashara yake ya kilimo.

 Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alikaa kwa muda wa saa tatu kwenye mazungumzo na kiongozi huyo wa Urusi akijaribu  kumshawishi kufufua makubaliano hayo ya usafirishaji nafaka kutoka Ukraine kupitia bandari tatu za eneo la bahari nyeusi,licha ya vita. 

Soma pia:Putin kukutana na Erdogan mjini Sochi

Mkutano huo uliofanyika katika mji wa Sochi, umefanyika katika wakati ambapo hivi karibuni Ukraine ilianzisha mashambulizi ya kujibu mapambano dhidi ya uvamizi wa Urusi.

Tangu rais Putin alipojiondowa katika mkataba huo wa usafirishaji nafaka ,Erdogan amekuwa  akiaahidi kufanya mipango ya kusaidia kuyafufua ili kuepusha mgogoro wa chakula katika baadhi ya nchi za Kiafrika,Mashariki ya Kati na Asia.


 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW