1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Erdogan: PKK kusalimisha silaha ni ukurasa mpya kwa Uturuki

12 Julai 2025

Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan, ametoa wito wa kuungwa mkono kikamilifu mpango wa kuwapokonya silaha wanamgambo wa Kikurdi, hatua iliyoanza kwa kusalimishwa kwa idadi ya silaha kadhaa kutoka kwa vikosi vya PKK.

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan akihutubia chama chake cha AKP mnamo Julai 17,2025 mjini Ankara
Rais wa Uturuki, Recep Tayyip ErdoganPicha: DHA

Wanamgambo thelathini wa PKK, jana walichoma moto silaha zao kwenye lango la pango moja kaskazini mwa Iraq, kuashiria hatua muhimu kuelekea kumaliza uasi uliodumu kwa miongo kadhaa nchini Uturuki.

Akihuwatubia wanachama wa chama chake cha AK mjini Ankara, Erdogan, amesema kufikia jana, kero la ugaidi lilianza mchakato wa kukamilika na kwamba leo, milango ya Uturuki iliyo imara imefunguliwa.

PKK yatangaza kuweka chini silaha

Rais huyo ameongeza kuwa hatua za hivi karibuni, zimeliunganisha taifa hilo na kwamba sasa bunge litatekeleza jukumu muhimu katika kuunda mfumo wa kisheria wa kukamilisha mchakato wa usalimishaji silaha.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW