Estonia: Umoja wa Mataifa kujadili uchokozi wa Urusi
22 Septemba 2025
Matangazo
Kitendo cha Urusi kukiuka usalama wa anga ya Estonia kilikosolewa vikali na Rais wa Marekani, Donald Trump.
Siku ya Ijumaa, vikosi vya Jumuiya ya Kujihami ya NATO, vilizizuia ndege tatu za kivita za Urusi chapa MiG-31, baada ya kuingia katika anga ya Estonia kwenye Ghuba ya Finland.
Hatua hiyo ilisababisha malalamiko ya uchokozi mpya unaoleta hatari katika nchi za NATO na Umoja wa Ulaya, madai yaliyokanushwa na Urusi.
Wakati huo huo, kikosi cha anga cha Ujerumani kimesema kimepeleka ndege mbili za kivita kuifatilia ndege moja ya kijeshi ya Urusi chapa IL-20m iliyoingia katika anga ya Bahari ya Baltic Jumapili.