Umoja wa Ulaya wakaribia kuidhinisha mkopo kwa Ukraine
22 Aprili 2026
Matangazo
Hungary iliuzuia uamuzi huo hadi Ukraine itengeneze bomba hilo. Baada ya Ukraine kukiri matengenezo yamekamilika Hungary ilipewa saa 24 kutoa idhini ya mwisho.
Kuondoka kwa Orban madarakani chanzo cha ahueni kwa Ukraine
Mgogoro huo ulisababisha mvutano kati ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, na kuchelewesha fedha ambazo Ukraine inazihitaji sana kufidia nakisi ya bajeti wakati vita na Urusi vinaendelea.
Endapo idhini ya mwisho ya mkopo huo itatolewa, Umoja wa Ulaya utaanza kutoa fedha hizo katika miezi ijayo. Mgogoro huo pia ulikuwa umezuia vikwazo vipya vya EU dhidi ya Urusi, ambavyo sasa vinaweza kuidhinishwa.