1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU, Marekani zashitushwa na uvunjaji wa haki Madagascar

17 Oktoba 2023

Umoja wa Ulaya na Marekani wameelezea hivi leo wasiwasi wao kuhusu matumizi ya nguvu kupita kiasi yaliyotumiwa kuzima maandamano ya upinzani nchini Madagascar, huku kukiwa na mvutano kabla ya uchaguzi wa rais.

Andry Rajoelina | madagassischer Präsident
Rais anayewania muhula mwengine madarakani nchini Madagascar, Andry Nirina Rajoelina.Picha: Lewis Joly/REUTERS

Upinzani unapinga mpango wowote wa kusalia madarakani kwa rais anayeondoka, Andry Rajoelina.

Katika taarifa ya pamoja, wawakilishi wa Umoja wa Ulaya, mashirika ya kimataifa pamoja na nchi nyingine saba zikiwemo Marekani, Ufaransa, Ujerumani na Japan, wameelezea wasiwasi wao kufuatia hali ya mvutano wa kisiasa nchini Madagascar, huku wakisisitiza umuhimu wa kuheshimu uhuru wa kujieleza na kukusanyika na kutoa wito kwa pande zote kushiriki katika mazungumzo.

Soma zaidi: Rais wa Madagascar ajiuzulu ili kugombea muhula wa pili

Wiki iliyopita, Mahakama ya juu nchini humo iliahirisha uchaguzi huo kwa wiki moja hadi Novemba 16, baada ya mgombea urais kujeruhiwa katika moja ya maandamano ya karibu kila siku katika kipindi cha wiki mbili, ambayo yamekitikisa kisiwa hicho kilichopo katika Bahari ya Hindi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW