Eu wajadili kuipatia mkopo mpya Ukraine
23 Februari 2026
Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wanakutana hivi leo mjini Brussels, kujadili mpango wa kuipatia mkopo mwingine Ukraine pamoja na awamu nyingine ya vikwazo dhidi ya Urusi.
Mazungumzo hayo yanafanyika siku moja kabla ya kumbukumbu ya miaka minne tangu Urusi ilipoivamia Ukraine Februari 24 mwaka 2022. Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas amesema mazungumzo ya Brussels yatalenga kuishinikiza zaidi Urusi.Trump kukutana uso kwa uso na Putin
''Bila shaka tunamajadiliano kuhusu Ukraine, kwahivyo ni wazi tutajadili kuhusu awamu ya 20 ya vikwazo lakini kama mnavyojuwa nyote, nafikiri hakutakuwa na hatua kubwa itakayopigwa leo kuhusiana na hili. Lakini bila shaka tutashinikiza suala hilo.''
Hungary imetishia mwishoni mwa Juma kuzuia mipango yote ya kuiwekea vikwazo Urusi na kuipatia mkopo wa yuro bilioni 90 Ukraine hadi pale usafirishaji wa mafuta kutoka Urusi kwenda Hungary utakaporuhusiwa.