Janga
EU yaandaa mkopo wa euro bilioni 90 kwa Ukraine
1 Aprili 2026
Matangazo
Fedha hizo bado zimekwama kufuatia upinzani wa Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban ambaye ni rafiki wa karibu wa rais wa Urusi Vladimir Putin.
Rais wa Halmashauri hiyo Ursula von der Leyen, amesema mkopo huo utafanikiwa kutolewa licha ya pingamizi hilo. Amesema hatua hiyo inatoa ujumbe wa wazi kabisa kwamba Ulaya iko tayari kusonga mbele.
Halmashauri hiyo imeandaa mswada wa kupitisha fedha hizo ambao unahitaji idhini ya pamoja ya nchi zote 27 za EU ili mkopo huo uanze kutolewa.
Chini ya mpango huo dola bilioni 45 zinazotarajiwa kutolewa mwaka 2026, dola bilioni 16.7 zinalenga kusaidia katika masuala ya bajeti ya Ukraine na dola bilioni 28.3 zikilenga kuimarisha sekta yake ya ulinzi pamoja na uwezo wake ikijumuisha utengenezaji wa droni.