1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU yamuwekea vikwazo kiongozi wa kijeshi wa RSF

21 Novemba 2025

Umoja wa Ulaya umewawekea vikwazo viongozi wakuu wa kundi la wanamgambo wa RSF nchini Sudan, kutokana na vita na mateso yanayoendelea dhidi ya raia katika vita vyake vya zaidi ya miaka miwili na jeshi la Sudan.

Sudan Al-Fascher 2025 | RSF
EU yamuwekea vikwazo kiongozi wa kijeshi wa RSF kutokana na mateso ya raia El Fasher Picha: Rapid Support Forces (RSF)/AFP

Mateso hayo yanajumuishamashambulizi yanayofanywa na kundi hilo katika mji wa El Fasher ulio magharibi mwa mkoa wa Darfur, uliodhibitiwa hivi karibuni na kundi hilo la RSF, baada ya kuzingirwa kwa miezi 18.

Vikwazo hivyo dhidi ya Abdel-Rahim Hamdan Dagalo vinafuatia vikwazo sawa na hivyo vilivyotolewa kwa kaka yake ambae ni kiongozi wa kundi RSF linalopambana na jeshi la Sudan,  Mohamed Hamdan Dagalo.

Baraza la masuala ya nje la Umoja wa Ulaya, limesema limemuwekea vikwazo Abdel-Rahim, kufuatia ukiukwaji wa haki za binaadamu uliofanywa na vikosi vyake katika mji wa El Fasher, Sudan

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW