1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU yasema vitisho havitakubaliwa kama hali ya kawaida

14 Novemba 2025

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas amesema leo kuwa Umoja huo utaendelea kufanya kazi kujilinda dhidi ya vitisho mseto.

Ubelgiji  Brüssel 2025 | Kaja Kallas
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja KallasPicha: Nicolas Tucat/AFP

Baada ya mkutano na mawaziri wa ulinzi wa Ujerumani, Ufaransa, Italia, Uingereza na Poland, Kallas amewaambia waandishi wa habari mjini Berlin kwamba Umoja huo wa Ulaya hauwezi kukubali vitisho hivyo kama hali mpya ya kawaida.

Uhamishaji wa wanajeshi na vifaa utahusisha wanachama wa EU

Pia amesema mpango wa uhamishaji wa vifaa na wanajeshi wa halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya utajumuisha kuunganisha rasilimali za usafiri za nchi wanachama na mapendekezo ya kuharakisha michakato ya kupatikana kwa vibali vya usafiri.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW