Lefunati Tambala, mbunifu wa samani kutoka Malawi, ameanzisha kampuni ya LeHome inayojikita katika utengenezaji wa fanicha za kifahari kwa kutumia raslimali za ndani, ufundi wa jadi na mitindo ya kisasa. LeHome inawakilisha mwelekeo mpya wa Afrika: kujenga uthabiti wa kiuchumi kupitia ubunifu wa ndani, uzalishaji wa hali ya juu na kujivunia utamaduni wa kitaifa.