1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

FIFA yapinga kauli ya Maradona

5 Julai 2018

Shirikisho la Soka Duniani FIFA limesema linazipinga kwa nguvu zote kauli za nyota wa zamani wa soka wa Argentina, Diego Maradona, kwamba ushindi wa timu ya Uingereza dhidi ya Colombia ni wizi.

Diego Maradona
Picha: picture-alliance/dpa/Tass/P. Kovalev

Aidha, Maradona alidai kwamba refa Mark Geiger hakuwa na viwango vya kusimamia mchezo huo. FIFA imesema kauli ya Maradona haikubaliki na haina msingi wowote. Uingereza ilishinda mechi hiyo kwa mikwaju ya penalti baada ya kumalizika dakika 120 za mchezo. FIFA pia imesema inafanya kila iwezalo kuhakikisha sheria ya Fair Play, uadilifu na heshima vinazingatiwa katika michuano ya Kombe la Dunia 2018.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW