1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaFinland

Finland ina matumaini ya kujiunga na NATO

30 Januari 2023

Finland imesema leo kuwa ina matumaini ya kujiunga na Jumuiya ya Kujihami NATO ikiwa pamoja na jirani yake Sweden licha ya matamshi ya rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki kuwa huenda itaidhinisha uanachama wa taifa hilo

Recep Tayyip Erdogan und Ulf Kristersson
Picha: Burhan Ozbilici/AP/picture alliance

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Finland Pekka Haavisto amewaambia wandishi habari mjini Helsinki kuwa dhamira ya serikali ya nchi hiyo ni kuona Finland na Sweden zinajiunga pamoja ndani ya NATOna msimamo huo haujabadilika.

Serikali ya Uturuki ambayo bado inajivutavuta kuridhia azimio la kuzikaribisha nchi hizo mbili ndani ya NATO, ilishupaza msimamo wake kuhusu Sweden baada ya kisa cha wiki iliyopita ambapo mwanasiasa wa mrengo mkali nchini Swedenaliichoma moto Quran Tukufu mbele ya ubalozi wa Uturuki mjini Stockholm.

soma pia:Erdogan ameashiria ataunga mkono kuikaribisha Finland NATO

Kufuatia kitendo hicho rais Erdogan alisema Sweden haiwezi tena kuitegemea Uturuki kuisaidia kupata unachama wa NATO.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW