1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Freiburg yafuzu 16 bora Stuttgart yayumba Ligi ya Ulaya

23 Januari 2026

Klabu ya Ligi Kuu ya Ujerumani Freiburg usiku wa kuamkia leo imeendeleza msururu wake wa kutofungwa katika mechi za Ligi ya Ulaya kwa kuilaza Maccabi Tel Aviv 1-0 na kujikatia tiketi ya hatua ya 16 bora.

DFB-Pokal 2025 | Achtelfinale | VfL Bochum vs. VfB Stuttgart | Stuttgarter Jubel nach dem zweiten Tor
Picha: Rene Nijhuis/MB Media Solutions/IMAGO

Christian Günter ndiye aliyefunga bao hilo la ushindi kunako dakika ya 82.

Kwengineko azma ya VfB Stuttgart ya kufuzu moja kwa moja kwenye hatua hiyo ya mtoano ya mashindano hayo ya Ulaya, imeingia doa baada ya kufungwa 2-0 na AS Roma ya Italia.

Kwa kushindwa huko Stuttgart sasa wanaishikilia nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi ya Ulaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW