SiasaHaiti
Genge lauwa 47 Haiti
25 Agosti 2026
Matangazo
Umoja wa Mataifa umesema idadi ya vifo inaweza kuongezeka huku tathmini ikiendelea.
Eneo la Kenscoff limekuwa likikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara ya magenge tangu mwaka jana, hali iliyowalazimu maelfu ya raia kuyahama makaazi yao.
Raia wanailaumu serikali na polisi kwa kushindwa kuzuia mauaji hayo, wakisema baadhi ya watu waliuawa karibu na kituo cha polisi bila kupata ulinzi wa kutosha.
Serikali ya Haiti imeelezea tukio hilo kuwa la kinyama na kuahidi kuimarisha usalama.
Hata hivyo, ongezeko la machafuko linaibua khofu kuhusu uwezo wa nchi hiyo kufanya uchaguzi uliopangwa kufanyika mwezi Desemba, ambao utakuwa wa kwanza katika kipindi cha miaka kumi.