MigogoroGhana
Ghana: Raia wetu 55 waliuawa katika vita nchini Ukraine
28 Februari 2026
Matangazo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ghana Samuel Okudzeto Ablakwa alifanya ziara wiki hii mjini Kyiv kujadili kuhusu hatima ya Waghana wawili waliokamatwa kwenye mstari wa mbele wa vita.
Hii ni idadi inayoongezeka katika miezi ya hivi karibuni ambapo nchi kadhaa za Afrika ikiwa ni pamoja na Kenya, Uganda, Afrika Kusini, na Gambia, zimekuwa zikigundua kuwa raia wao walidanganywa kupewa ajira na mishahara minono na badala yake wakajikuta wamesajiliwa katika jeshi la Urusi, huku wengi wakiuawa au kukamatwa kwenye uwanja wa vita.