Filamu hii fupi inahusu mtu mwenye ujuzi mjini Mwanza nchini Tanzania. Amekuwa akitengeneza mazulia yenye nembo na kuyauza kwa mahoteli makubwa, afisi za serikali na hata za kibinafsi mjini humo. Ni maarufu kwa kutumia malighafi inayopatikana mjini humo na sindano kutengeneza mazulia kutumia mikono yake mwenyewe.