1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guinea ya Ikweta yaiomba ICJ kuyakataa madai ya Gabon

30 Septemba 2024

Guinea ya Ikweta imewaomba majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) hii leo kukataa madai ya Gabon kwamba visiwa kadhaa vinavyoweza kuwa na utajiri wa mafuta katika Ghuba ya Guinea ni vyake.

Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) mjini The Hague, Uholanzi.
Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) mjini The Hague, Uholanzi.Picha: Daniel Kalker/picture alliance

Nchi hizo jirani na wazalishaji wa mafuta barani Afrika zimeiomba mahakama ya ICJ kuusuluhisha mzozo wa muda mrefu kuhusu kisiwa kidogo cha Mbanié kilicho kwenye pwani ya Gabon na chenye ukubwa wa chini ya kilomita moja.

Mzozo huo umekuwa ukiendelea tangu mwaka 1972, wakati jeshi la Gabon lilipowafukuza wanajeshi wa Guinea ya Ikweta kutoka Mbanié.

Soma zaidi: Kiongozi wa kijeshi wa Gabon ziarani Burundi

Kwa upande wake, tangu wakati huo Gabon imewaweka wanajeshi wake kwenye eneo hilo lisilo na watu kwenye kisiwa hicho chenye ukubwa wa ekari 74 tu.

Mahakama ya mjini The Hague inatarajiwa kutoa uamuzi wake mwaka ujao.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW