1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres aelezea aitaka dunia kuachana nishati ya visukuku

17 Januari 2024

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ni muhimu kwa ulimwengu kuondokana na matumizi ya nishati ya visukuku ili kuepuka janga la mazingira duniani.

Schweiz | Weltwirtschaftsforum in Davos - Antonio Guterres, UN-Generalsekretär
Picha: Gian Ehrenzeller/KEYSTONE/picture alliance

Akizungumza katika kongamano la kiuchumi la dunia mjini Davos Uswisi, Guterres ameeleza kuwa dunia haina budi kuondokana na matumizi ya nishati ya visukuku na anatumai kuwa, dunia haitochelewa kufanya hivyo.

Takriban mataifa 200 yalikubaliana kwa sauti moja katika mkutano wa kilele wa mazingira wa COP28 mwezi uliopita kuanza kupunguza matumizi ya nishati ya visukukuu ili kuepusha janga baya la mazingira.

COP28 yafikia makubaliano kuachana na nishati za visukuku

Makubaliano hayo, yaliyofikiwa baada ya wiki mbili za mazungumzo, yalikuwa na nia ya kutuma ujumbe kwa wawekezaji na viongozi wa siasa duniani kuachana na nishati ya visukuku.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW