1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres aonya juu ya kuboreshwa kwa silaha za nyuklia

30 Agosti 2023

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametahadharisha kuwa ongezeko la kutoaminiana kimataifa pamoja na juhudi za baadhi ya mataifa kuboresha silaha zao za nyuklia ni "kichocheo cha maangamizi."

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio GuterresPicha: Grigory Sysoev/SNA/IMAGO

Katika taarifa ya kuadhimisha siku ya kimataifa ya kupambana na majaribio ya nyuklia, Guterres amesema kwamba kuna silaha za nyuklia zipatazo 13,000 duniani kote, na kueleza umuhimu wa kupiga marufuku majaribio ya nyuklia kuelekea ulimwengu usiokuwa na silaha za nyuklia.

Mkataba wa kupiga marufuku majaribio ya nyuklia una nchi wanachama 196 huku 186 kati yao wakiutia saini na 178 kuuidhinisha, zikiwemo nchi nane katika muda wa miezi 18 iliyopita. 

Katika mkutano wa kuadhimisha siku hiyo, hapakuwa na dalili kuwa nchi hizo nane - Marekani, China, Misri, Israel, Korea Kaskazini, India na Pakistan - zinaelekea kuutekeleza mkataba huo.

Umoja wa Mataifa ulitangaza Agosti 29 kila mwaka kuwa Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Majaribio ya Nyuklia.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW