1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Guterres aonya kuhusu mwelekeo hatari wa vita nchini Ukraine

29 Mei 2026

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametahadharisha kuhusu mwelekeo wa vita vinavyoendelea nchini Ukraine na kusema, "ongezeko la mapigano linaloshuhudiwa kwa sasa lina hatari ya kutoka nje ya udhibiti."

Marekani New York 2025 | Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António GuterresPicha: Eskinder Debebe/Xinhua/IMAGO

Guterres ameliambia baraza la usalama kwamba "mashambulizi makubwa yaliyoanzishwa na Urusi kote nchini Ukraine katika siku za hivi karibuni yanaonyesha uzito na hali ya hatari kwa wakati huu."

Amesema kuwa hali ya kibinadamu inaendelea kuzorota kwa kasi, na kurejea taarifa za Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu, ambazo zinaonyesha kuwa tangu uvamizi wa Urusi kuanza Februari 2022, zaidi ya raia 15,000 wameuawa nchini Ukraine – wakiwemo watoto 800.

Aidha, ripoti kutoka Urusi zinaonyesha ongezeko la vifo vya raia ndani ya maeneo yanayodhibitiwa na nchi hiyo, vikiwemo vifo vya watoto.

Katibu Mkuu huyo amesisitiza umuhimu wa kuchukua hatua za dharura za kupunguza uhasama, akitoa mwito wa "usitishaji kamili na usio na masharti wa mapigano mara moja.” Amesisitiza kuwa njia pekee ya kuzuia madhara zaidi ni kurejesha mazungumzo ya kidiplomasia na kuhakikisha kuwa sheria za kimataifa za kibinadamu zinaheshimiwa na pande zote.

 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW