1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres atoa mwito wa usitishwaji wa mapigano Sudan

28 Oktoba 2025

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, ametoa mwito wa mazungumzo ya amani kufanyika mara moja ili kusitisha mapigano yanayoendelea Sudan.

Malaysia Kuala Lumpur 2025 | UN-Generalsekretär Guterres beim ASEAN-UN-Gipfel
Picha: Chalinee Thirasupa/Pool/AFP

Mwito wa Guterres unatolewa baada ya wanamgambo wa RSF kuuteka mji wa El Fasher jana Jumatatu. Katika taarifa, msemaji wa katibu huyo mkuu wa Umoja wa Mataifa, Stephan Dujarric, amesema Guterres analitaka jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF kuwasiliana na mjumbe wake wa Sudan Ramtane Lamamra,haraka kwa ajili ya kuchukua hatua za haraka za kufikia makubaliano.

Wakati huo huo, Umoja wa Afrika umelaani visa vya ''Ukatili'' na "uhalifu wa kivita" vinavyoripotiwa huko El Fasher.

Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya umoja huo, Mahmoud Ali Youssouf kupitia taarifa aliyoitoa kwenye mtandao wa kijamii wa X, amesema ana wasiwasi kuhusu machafuko na madai ya mauaji ya kikabila yanayoendelea huko El Fasher.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW