1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Haiti yaomba msaada wa kukabiliana na vurugu za magenge

26 Septemba 2025

Mkuu wa baraza la mpito la urais nchini Haiti Laurent Saint-Cyr, ameyaomba mataifa ya dunia kuisaidia nchi yake kukabiliana na kile alichokitaja kuwa vita dhidi ya ghasia za magenge na njaa iliyoenea.

Haiti Port-au-Prince 2025 | Laurent Saint-Cyr
Mkuu wa baraza la mpito la urais nchini Haiti Laurent Saint-CyrPicha: Clarens Siffroy/AFP

Akilihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, Saint-Cyr, amesema hatua za haraka zinahitajika kwa sababu watu wanakufa kila siku nchini Haiti.

Saint-Cyr ameongeza kuwa ni muhimu kusema kuwa Haiti inakabiliwa na vita kati ya wahalifu wanaotaka kulazimisha vurugu kama utaratibu wa kijamii na watu wenye silaha wanaopigania utu na uhuru wa binadamu.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW