1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaMarekani

Hali ya hatari yatangazwa New York kufuatia mafuriko makubwa

30 Septemba 2023

Hali ya hatari imetangazwa katika jiji la New York kutokana na upepo mkali uliondamana na mvua kubwa iliyosababisha mafuriko ya ghafla.

Starkregen Überschwemmung New York
Mafuriko yameukumba mji wa New York, MarekaniPicha: Jake Offenhartz/picture alliance/dpa/AP

Barabara za chini ya ardhi, mitaa na barabara kuu za mji huo zimefurika huku kituo kimoja cha uwanja wa ndege wa LaGuardia kikifungwa.

Gavana wa jimbo hilo Kathy Hochul amesema mvua ya hadi sentimita 12.7 imenyesha usiku kucha katika baadhi ya maeneo huku ikitarajiwa kuendelea.

Bi Hochul amewahimiza watu kusalia majumbani na kamwe "kutojaribu kusafiri kwenye barabara zilizojaa maji."

Licha ya kutotangazwa vifo au majeruhi hadi sasa, baadhi ya wakaazi wameingiwa na hofu.

Hali ya hatari pia imetangazwa katika mji wa Hoboken, jimbo la New Jersey.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW