Hali ya kisiasa katika kisiwa cha Nzouani baada ya kufanya uchaguzi wa rais kwa lazima
14 Juni 2007Matangazo
Uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Jumapili iliyopita lakini kuahirishwa hadi tarehe 17 mwezi huu kwa sababu za kiusalama. Tume ya uchaguzi ya Nzouani ilikiuka agizo hilo na kufanya uchaguzi na kumtangaza raia wa zamani wa kisiwa hicho Mohamed Bakary mshindi. Mohamed Bakary aliingia madarakani baada ya kupindua serikali mwezi Agosti mwaka 2001 na kuongoza kwa muhula wa miaka mitano mwaka uliofuatia. Hasa hatua za kijeshi zina maana gani dhidi ya Nzouani? Thelma Mwadzaya alimuuliza Ibrahim Abdalla mshauri wa rais wa serikali kuu ya Komoro Abdalla Sambi.