1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas yakanusha kujiondoa kwenye mchakato wa mazungumzo

Angela Mdungu
14 Julai 2024

Kundi la Hamas limekanusha taarifa za awali kuwa mazungumzo ya kusitisha vita kati yake na Israel yamevunjika.

Kiongozi wa Kundi la Hamas Ismail Haniyeh
Kiongozi wa Kundi la Hamas Ismail HaniyehPicha: Vahid Salemi/AP Photo/picture alliance

Kundi hilo limesema mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja bado yanaendelea licha ya mamlaka ya afya inayodhibitiwa na kundi hilo kusema kuwa mashambulizi ya anga ya Israel yaliwauwa watu 90 jana Jumamosi.

Awali, Israel ilisema kuwa mashambulizi hayo yalimlenga kiongozi wa tawi la kijeshi wa Hamas, Mohammed Deif. Hata hivyo muwakilishi wa kundi hilo katika mji Mkuu wa Lebanon, Beirut amesema leo kuwa, Deif hakuuwawa katika tukio hilo.

Hayo yakijiri, Jeshi la Israel limesema kuwa limemuuwa kamanda wa kikosi cha kijeshi cha Hamas katika mji wa Khan Younis Rafa Salama, katika shambulio la anga la Jumamosi. Shambulio hilo ndilo lililotajwa kumlenga kiongozi wa tawi la kijeshi wa Hamas, Mohammed Deif.

 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW