1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HAMBURG: Mchango wa NATO uimarishwe Afghanistan

24 Septemba 2006

Katibu Mkuu wa Shirika la Kujihami la NATO,Jaap de Hoop Scheffer ametoa wito kwa shirika hilo kupanua ujumbe wake nchini Afghanistan.Kwa mujibu wa makala iliyochapishwa na gazeti la Kijerumani “Bild am Sonntag,” De Hoop amesema,Afghanistan kamwe isiwe tena kambi ya kutoa mafunzo kwa magaidi.Siku moja kabla ya bunge la Ujerumani kupiga kura ikiwa irefushe mamlaka ya kubakia na vikosi vya amani nchini Afghanistan,De Hoop ameitaka serikali ya Berlin itoe mchango zaidi katika vikosi vya kimataifa nchini Afghanistan.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW