1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HANOI : Kimbunga Xangsane kinakaribia pwani ya Vietnam

30 Septemba 2006

Nchini Vietnam,kiasi ya watu 200,000 wamehamishwa kutoka eneo la pwani sehemu za kati za nchi hiyo ili kujiepusha na kimbunga kinachokuja kutoka Ufilipino.Kimbunga kilichopewa jina “Xangsane” kimeua si chini ya watu 62 nchini Ufilipino na wengine 68 bado hawajulikani walipo.Hicho ni kimbunga kibaya kabisa kupata kutokea Ufilipino tangu mwongo mmoja na kimewaacha mamilioni ya wakazi bila ya umeme katika kisiwa kikuu cha Luzon kaskazini mwa nchi.Maafisa wamesema,kama watu wapatao 90,000 hawawezi kurejea majumbani mwao kwa sababu ya hofu kuwa mmomonyoko wa ardhi huenda ukangoa nyumba.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW