1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HARARE: Maripota 2 wa Kingereza waachiliwa huru Zimbabwe

16 Aprili 2005

Waandishi habari wawili wa Kingereza waliofikishwa mahakamani nchini Zimbabwe kwa mashtaka ya kuripoti uchaguzi wa mwezi uliopita bila ya ruhusa,wameachiliwa huru.Hakimu,Never Diza amesema,waendesha mashtaka wameshindwa kuthibitisha kuwa Toby Harnden na Julian Simmonds wamefanya kazi nchini,kinyume na sheria.Watu hao wawili waliokamatwa karibu na mji wa Harare siku ya uchaguzi,waliachiliwa kwa dhamana baada ya kuwekwa jela kwa wiki mbili.Waingereza hao wamesema walikuwa wakiizuru Zimbabwe kama watalii.Wapelelezi wa serikali walizuia kompyuta za mkono na kamera,lakini hawakuweza kufasiri hati-mkato.Kamera nayo haikuwa na picha.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW