1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HARARE: Mugabe asema Zimbabwe itafanya uchaguzi huru.

25 Machi 2005

Serikali ya Zimbabwe imeanza matayarisho ya kiusalama huku uchaguzi wa bunge wa nchi hiyo ukikaribia.

Rais Robert Mugabe amesema kuwa serikali yake inafanya kila juhudi ili kuwepo na uchaguzi huru na wa haki ambao unasubiriwa kwa hamu na jamii ya kimataifa.

Chama cha upinzani cha Zimbabwe MDC kinasema kuwa chama tawala cha ZANU FP kinatumia vibaya vyombo vya habari kujifanyia kampeni.

Uchunguzi unaonyesha kuwa visa vya vurugu za kisiasa nchini Zimbabwe vimepungua huku uchaguzi ukitarajiwa kufanyika Machi 31.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW