1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiAfrika

Hatma ya mkataba wa AGOA bado kitendawili

30 Septemba 2025

Marekani imeashiria kuurefusha mkataba wa AGOA japo kuna wasiwasi barani Afrika kuhusu hatma ya mkataba huo wa kibiashara

Mkutano wa AGOA wa 20 ulifanyika Afrika Kusini ukijadili pamoja na mengine, uungaji mkono wa uchumi wa maendeleo,viwanda na kujenga nafasi bora za ajira
Mkutano wa AGOA wa 20 ulifanyika Afrika Kusini ukijadili pamoja na mengine, uungaji mkono wa uchumi wa maendeleo,viwanda na kujenga nafasi bora za ajira

Mkataba wa kibiashara wa AGOA, unaotoa fursa ya kusaidia ukuaji barani Afrika, unafikia tamati leo Jumanne huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu iwapo Marekani itaurefusha.

Kumalizika kwa mkataba huo kunahatarisha maelfu ya ajira barani Afrika, ikiwemo nchini Kenya ambako AGOA imeimarisha sekta ya utengenezaji wa vitambaa na mavazi, na kuiwezesha kushindana na wazalishaji kutoka mataifa ya Asia kama Bangladesh na Vietnam.

Utawala wa Rais Donald Trump umesema unaunga mkono kurefusha mkataba huo kwa mwaka mmoja. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000, AGOA imefanikisha maelfu ya bidhaa kutoka mataifa ya Afrika yaliyokidhi vigezo kuuzwa katika masoko ya Marekani bila ushuru.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW