Usajili wa maeneo ya Palestina wakosolewa
16 Februari 2026
Hatua ya serikali ya Israel kuidhinisha mchakato wa kusajili ardhi kwenye Ukingo wa Magharibi, imelaumiwa na mataifa ya Kiarabu na wakosoaji waliouita "unyakuzi mkubwa wa ardhi" ambao ungeharakisha pia unyakuzi wa ardhi hiyo ya Palestina.
Misri, Qatar na Jordan wamekosoa hatua hiyo wakiitaja kuwa haramu na inayokiuka sheria ya kimataifa.
Kwenye taarifa yao, Misri imesema uamuzi huo ni hatari na unaolenga kudhibiti maeneo yanayokaliwa na Kipalestina, huku Qatar ikisema ni uamuzi unaolenga kuibadilisha ardhi ya Ukingo wa Magharibi kuwa mali ya serikali, na ambao utawanyima Wapalestina haki zao.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel ilisema ni hatua ambayo ingewezesha "ufafanuzi wa wazi na wa kina wa haki za kutatua migogoro" na ilihitajika kufuatia usajili haramu wa ardhi katika maeneo yanayodhibitiwa na Mamlaka ya Palestina.