1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hillary Clinton awasifu waasi wa Libya

19 Oktoba 2011

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton, amewasifu waasi wa Libya kwa kufanikiwa kumng’oa madarakani Kanali Muammar Gaddafi.

Hillary Rodham ClintonPicha: dapd

Mwanadiplomasia huyo alito ahadi kuwa Marekani itafanya kila iwezalo kulisaida baraza la mpito la waasi wa Libya kurejea katika mkondo wa demokrasia.

Akizungumza na viongozi wa Baraza hilo mjini Tripoli; Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton, alisema kuwa Walibya waliupiga vita udikteta uliokuwako na wamefanikiwa kurejesha haki za taifa lililo huru.

Mapambano makali yaendelea Sirte: ngome ya mwisho ya Kanali Gaddafi iliyosalia.Picha: picture alliance / dpa

Bibi Clinton alisisitiza kuwa Marekani itauunga mkono mfumo utakaoyapa kipa umbele masuala ya demokrasia na makundi yanayotaka kuivuruga mipango hiyo yatalazimika kupambana na Walibya wenywewe.

Kanali Moammar Gadhafi, bado hajulikani aliko.Picha: dapd

Hillary Clinton aliwasili kwenye mji mkuu wa Libya wa Tripoli, akiwa katika ziara ambayo haikutarajiwa. Wakati huohuo mapambano makali yanaripotiwa kuendelea mjini Sirte alikozaliwa Kanali Gaddafi. Sirte ni ngome yake ya mwisho muhimu iliyosalia.

Mwandishi: Mwadzaya,Thelma-ZPR

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW