1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaHonduras

Honduras na China kuanzisha tena uhusiano wa kidiplomasia

26 Machi 2023

China na Honduras zimetangaza leo kurejesha rasmi uhusiano wao wa kidiplomasia, huku Taiwan ikiishutumu Beijing kwa kutumia "shinikizo na vitisho" kuwarubuni washirika wake wachache waliosalia.

China I China und Honduras nehmen diplomatische Beziehungen auf
Picha: Greg Baker/AFP

Tangazo la China kuhusu hatua hiyo linajiri muda mfupi baada ya Honduras kusema kuwa imesitisha rasmi uhusiano na Taiwan, ambayo imepoteza washirika kadhaa wa Amerika Kusini katika miaka ya hivi karibuni.

Mabadiliko hayo, yanaripotiwa siku chache tu baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Honduras Enrique Reina kufanya ziara mjini Beijing, na kuiacha Taiwan ikiwa na nchi 13 tu zinazoitambua rasmi kuwa huru.

Soma pia: China imerejelea vitisho vya kuishambulia Taiwan

Waziri Reina amesema Taiwan ni sehemu isiyoweza kutengwa kunako eneo la China.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW