Hoteli ya Kempinski haitoendeshwa tena Zanzibar
16 Mei 2011Matangazo
Mmiliki wa hoteli hiyo ya kifahari sasa anatafuta kampuni nyingine kusimamia uendeshaji wa hoteli hiyo. Na ilivokuwa watalii wenye kujiweza wanaoelekea Visiwani Zanzibar makaazi yao huwa katika hoteli hiyo, Othman Miraji alizungumza hivi punde na katibu mkuu wa wizara ya habari, utamaduni, utalii na michezo ya Zanzibar, Dr Ali Mwinyikai, kupata zaidi kuhusu mada hii...