Sheria na HakiAfrika
Hukumu kesi dhidi ya Joseph Kabila yaahirishwa Kongo
13 Septemba 2025
Matangazo
Mahakama hiyo ambayo iliisikiliza kesi bila Kabila kuwepo mwezi Julai, ilikubali kufungua tena kesi hiyo baada ya wito wa dakika za mwisho wa kutaka mashtaka yaainishwe kuwa ya kufanya Ujasusi.
Kabila aliingia madarakani mwaka 2001 na kuiongoza Kongo hadi 2019. Aliondoka nchini humo mwaka 2023 na alirejea mwezi Mei mwaka huu ambapo alifikia mashariki mwa Goma, eneo linalokaliwa na waasi wa M23.Bunge la Kongo lilimuondolea kinga ya mashtaka ili kuruhusu ashtakiwe. Kando ya uhaini, Kabila anashutumiwa kwa uhalifu wa kivita na kushirikiana na waasi wa waasi wa M23 ambao wanashikilia maeneo makubwa ya eneo la mashariki mwa Kongo lenye utajiri mkubwa wa rasilimali.