1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IAEA: Hakuna hatari Zaporizhzhia baada ya umeme kukatika

1 Oktoba 2025

Shirika la Umoja wa Mataifa la kudhibiti matumizi ya nishati ya nyuklia, IAEA limesema hakuna hatari iliyojitokeza katika kinu cha nyuklia cha Zaporizhzhia, baada ya umeme kukatika tangu wiki iliyopita.

Ukraine | Kinu cha nyuklia cha Zaporizhzhia
Hakuna hatari iliyojitokeza katika kinu cha nyuklia cha ZaporizhzhiaPicha: Alexei Konovalov/ITAR-TASS/IMAGO

IAEA imesema hakuna hatari katika kinu hicho kinachodhibitiwa na Urusi nchini Ukraine kwa sababu jenereta za dharura zinaendelea kufanya kazi.

Shirika hilo limesema hiyo sio hali inayopaswa kuendelea kwa kuzingatia suala la usalama wa nyuklia.

Siku ya Jumanne, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alionya kuhusu kitisho kinachoweza kutokea akisema hali katika kinu hicho ni mbaya.

Aidha, shirika la habari la Urusi, RIA limetangaza Jumatano kuwa uongozi uliowekwa na Urusi katika kinu hicho umesema usambazaji wa umeme wa dharura unatosha.

Hata hivyo, wamesema kuanza tena usambazaji umeme kupitia njia ya Dneprovskaya, hakuwezakani kutokana na mashambulizi ya Ukraine.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW