1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ibada ya kitaifa ya kumuaga Odinga yafanyika Nairobi

17 Oktoba 2025

Ibada rasmi ya kitaifa ya aliyekuwa waziri mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga, imefanyika jijini Nairobi. Viongozi na raia walikusanyika kwenye uwanja wa Nyayo kumfanyia marehemu kigogo huyo sala ya mwisho ya kitaifa.

Kenya Nairobi 2025 | Mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga
Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga lilipofika kwenye ibada ya kitaifa ya wafu Ijumaa Oktoba 17, 2025Picha: Andrew Kasuku/AP Photo/picture alliance

Wakati jeneza la hayati Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga lilipowasili kwenye uwanja wa Nyayo jijini Nairobi, mayowe, vilio, na firimbi zilisikika kutoka kwa umati muliokuwepo uwanjani hapo. Vikosi vya taifa viliungana na kwa pamoja kuchukua usukani ili kumpa marehemu Raila Odinga heshima kamili za kiongozi wa taifa.

Viongozi wa mataifa mbalimbali walipata fursa kutoa heshima zao za mwisho akiwemo rais mstaafu wa Tanzania Jakaya Kikwete Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud, mabalozi na wageni rasmi.

Usalama watawala kwenye shughuli ya ibada

Binti ya Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga, Rosemary Odinga, akiwahutubia waombolezaji wakati wa ibada ya mazishi yake kwenye Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi, Kenya, Oktoba 17, 2025.Picha: Monicah Mwangi/REUTERS

Mapema asubuhi, wabunge, mawaziri na viongozi serikalini walipata fursa kumuaga rasmi hayati naibu waziri mkuu wa zamani Raila Odinga kwenye majengo ya bunge. Umati ulitulia pindi wanawe walipopanda jukwaani kuzungumza na bintiye hayati Rosemary Odinga aliwashukuru waombolezaji kwa kumuenzi kigogo huyo.

Shughuli hiyo ilitibuka siku ya Alhamisi kwani umati wa waombolezaji uliojitokeza uliwazidi nguvu maafisa wa usalama. Siku ya Ijumaa, usalama uliimarishwa katikati ya jiji la Nairobi na ugani Nyayo kwenyewe.

Mjane Mama Idah Odinga aliwarai wakenya kusameheana na kuimarisha uhusiano katika jamii. Maziko rasmi yamepangwa kufanywa siku ya Jumapili nyumbani kwake Bondo kaunti ya Siaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW