1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ICC yatoa waranti ya kukamatwa viongozi waandamizi wa Urusi

25 Juni 2024

Mahakama ya Kimaitaifa ya ICC imetoa waranti ya kukamatwa kwa waziri wa zamani wa ulinzi wa Urusi, Sergei Shoigu na jenerali wa juu, Valery Gerasimov, wanaodaiwa kuhusika na uhalifu katika vita vya Urusi Ukraine.

Urusi lSergei Shoigu
waziri wa zamani wa ulinzi wa Urusi, Sergei Shoigu Picha: Russian Defence Ministry/dpa/picture-alliance

Shoigu aliondolewa kwenye wadhifa wake wa waziri wa ulinzi mwezi uliopita, na kuteuliwa kuwa katibu wa baraza la usalama la Urusi lenye  nguvu kubwa, katika mabadiliko muhimu zaidi kufanywa na Rais wa Urusi Vladimir Putin tangu kuanza kwa vita mwaka 2022.

Mahakama ya ICJ yatazamiwa kutoa uamuzi kuhusu vita vya Gaza

Waukraine kudai fidia kwa uharibifu wa vita vya Urusi

Taarifa ya ICC kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa majaji wamebaini kuwa pasi na shaka washukiwa hao wawili wamehusika katika mashambulizi yaliotekelezwa na jeshi la Urusi, dhidi ya miundombinu ya umeme ya Ukraine kati ya Oktoba 10, 2022 hadi Machi 9, 2023.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW