1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Idadi ndogo ya wapiga kura yashuhudiwa nchini Tanzania

29 Oktoba 2025

Idadi ndogo ya wapiga kura imejitokeza katika jiji kuu la Tanzania, Dar es Salaam, leo kwa zoezi la uchaguzi huku wapinzani wakuu wa Rais Samia Suluhu Hassan wakiwa aidha wamefungwa jela ama kuzuiwa kugombea.

Tanzania Stone Town 2025 | Shughuli ya uchaguzi
Zoezi la kupia kura mjini Stone Town, ZanzibarPicha: Marco Longari/AFP

Vituo vya kupiga kura katika baadhi ya maeneo yenye shughuli nyingi zaidi jijini humo vilikuwa tupu saa moja baada ya kufunguliwa, licha ya kuwa na shughuli nyingi wakati kama huo wakati wa chaguzi zilizopita.

Haya yameripotiwa na shirika la habari la AFP.

Watu kuhamasishwa kupiga kura

Afisa mmoja kutoka chama tawala, Chama cha Mapinduzi, CCM wilayani Temeke  Dar es Salaam, aliyezungumza na AFP kwa sharti la kutotajwa jina, amesema watawahamasisha watu mitaani na majumbani kutoka na kupiga kura.

Awali shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International lilaani kile ilichokitaja kuwa "wimbi la ugaidi" kabla ya uchaguzi huo ikiwa ni pamoja na "kutoweka na kuteswa kwa watu pamoja na mauaji ya kiholela ya viongozi wa upinzani na wanaharakati.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW