1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Idadi ya vifo vya mafuriko nchini Kenya yaongezeka

Saleh Mwanamilongo
2 Mei 2026

Watu wasiopungua kumi wamefariki nchini Kenya kutokana na mvua kubwa zilizosababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi katika maeneo mbalimbali nchini humo, kwa mujibu wa polisi.

Kenya | Nairobi 2026 – Mafuriko katika soko la vipuri vya magari lililopo Barabara ya Grogan
Kenya | Nairobi 2026 – Mafuriko katika soko la vipuri vya magari lililopo Barabara ya GroganPicha: Boniface Muthoni/SOPA Images/Sipa USA/picture alliance

Vifo saba vimeripotiwa mashariki mwa nchi, huku madaraja mawili yakiharibiwa katika kaunti za Kwale na Kitui. Maporomoko ya ardhi pia yameripotiwa katika kaunti ya Elgeyo Marakwet eneo la Bonde la Ufa.

Mamlaka zinasema kiwango kikubwa cha mvua na ardhi iliyojaa maji kimeongeza hatari ya mafuriko. Usafiri umeathirika baada ya baadhi ya barabara kufungwa kutokana na maporomoko ya ardhi.

Shirika la Msalaba Mwekundu linasema kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa za watu kupotea na familia kukwama katika eneo la Mukuru Kwa Njenga jijini Nairobi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW