1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiAsia

Idadi ya watu China yapungua kwa mwaka wa pili mfululizo

17 Januari 2024

Idadi ya watu nchini China imepungua kwa mwaka wa pili mfululizo na kuongeza wasiwasi juu ya ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo ambao ni wa pili kwa ukubwa duniani.

China | Beijing
Idadi ya watu China inasemekana kupungua Picha: Mark Schiefelbein/AP Photo/picture alliance

Takwimu zilizotolewa leo zimeonyesha kuwa nchi hiyo ya Asia Mashariki ilikuwa na idadi ya watu wapatao bilioni 1.409 kufikia mwisho wa mwaka 2023, idadi hiyo ikiwa pungufu ya watu milioni 2.08 kutoka mwaka 2022.

Pia, idadi ya vifo vilivyoripotiwa mwaka jana viliongezeka kwa asilimia 6.6, sawa na watu milioni 11.1, kiwango hicho kikiwa cha juu zaidi tangu mwaka 1974 wakati wa mapinduzi ya utamaduni.

China yatangaza kupungua kwa idadi ya watu wake

Hata hivyo, wataalamu wanatoa hoja kwamba upungufu huo wa idadi ya watu ulitarajiwa kutokana na kuongezeka kwa tabaka la watu wanaoishi mjini na pia kiwango kidogo cha watoto wanaozaliwa.

China imeshuhudia kiwango kidogo cha watoto wanaozaliwa kwa miongo kadha sasa- hasa baada ya kuweka sera yenye utata ya kuwataka watu kuwa na mtoto mmoja tu.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW