1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IMF yaipa Burkina Faso mkopo wa dola milioni 302

22 Septemba 2023

Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF limeidhinisha mpango wa miaka minne wa mkopo wa dola milioni 302 kwa Burkina Faso.

Burkina Faso | Ibrahim Traore
Kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso Ibrahim TraorePicha: AA/picture alliance

IMF imesema mkopo huo utaipa Burkina Faso nafasi ya kuyatekeleza matumizi yake ya kipaumbele baada ya nchi hiyo kukabiliwa na mapinduzi mara mbili tangu mwezi Januari mwaka jana.

Burkina Faso pia inakabiliwa na hali mbaya ya usalama na kiuchumi iliyochangiwa na vita vya nchini Ukraine, misukosuko iliyosababishwa na janga la COVID-19, ukame, migogoro na uhaba wa chakula.

Soma: Ibrahim Traore kuapishwa Ijumaa kama rais wa mpito

IMF imesema majanga hayo yamevuruga uchumi na ustawi katika taifa hilo la Afrika magharibi.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi linakadiria kuwa zaidi ya watu milioni mbili wamegeuka kuwa wakimbizi wa ndani kutokana na kutokuwepo kwa usalama nchini Burkina Faso.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW